1

Kamati Kuu ya CCM (CC) iliyoketi leo hii chini ya Mwenyekiti Jakaya Kikwete imempongeza Rais Magufuli kwa mapambano aliyoyaanzisha na kumtia moyo kuwa CCM,kwa ujumla wake,iko pamoja naye.

Lakini,CC imemshauri na kumtaka Rais Magufuli kujiridhisha vya kutosha kabla ya kutumbua majipu mbalimbali ya kitaifa. Imesemwa kuwa nchi yaweza kuendeshwa kwa majungu na hivyo wananchi kuishi kwa visasi na kuchongeana. Ni kama CC imemfunga Speed Governor Rais Magufuli 'kimtindo'.

Pia,CC imemtaka kuwa makini na teuzi zake za sasa na zijazo. Imedhihirika leo kuwa Rais Magufuli alikuwa akisubiri kikao cha CC ili kuteua na kutangaza Mawaziri. Sasa mambo yatafanyika!

ZINGINE KALI ZAIDI BOFYA HAPA CHINI USIPITWE

Post a Comment

WRITE YOUR COMMENTS HERE

 
Top