Latiffah Naseeb Abdul a.k.a Tiffah Dangote au kama wazazi wake Diamond na Zari wanavyomuita ‘The African Royal Princess’, anaendelea kupata umaarufu kwenye mitandao ya kijamii akiwa na umri wa siku moja tu.

Kupitia akaunti yake ya Instagram @princess_tiffah iliyofunguliwa jana baada ya kuzaliwa, imepostiwa picha ya kwanza ya baba na mwana, Diamond akiwa na mtoto wake kitandani. Hata hivyo mtoto anaonekana mkono tu.

Hii ndio caption iliyoandikwa katika post hiyo:

My Dad Couldn’t seep last night, he was staring at me the whole night #MyFirstDayInTheStateHouse”.

Mpaka sasa akaunti ya @princess_tiffah imefikisha followers 44,357 ikiwa ni siku moja toka ifunguliwe.
 
Top