0




Bondia Floyd Mayweather ambaye kwa sasa anafurahia kwa kufanikiwa kulinda rekodi yake ya kutopoteza pambano hata moja katika mapambano yake 50 baada ya kufanikiwa kumpiga Bondia Mc Gregor kwa Technical Knock Out (TKO) round ya 10 katika pambani la round 12.

Mayweather ameripotiwa na mtandao wa dailymail.co.uk kuwa pambano lake na Mc Gregor ndio pambano lake la mwisho na ameamua kustaafu mchezo wa ngumi, japokuwa kuna watu wanaweza kufikiria kuwa atarudi tena ulingoni.

Hata hivyo Mayweather katika interview hiyo amethibitisha kuwa na wasichana saba katika mahusiano ya kimapenzi kwa sababu kuwa na msichana mmoja ni sawa na kuwa hauna kabisa.

“Nina wasichana wangapi? kama saba hivi ambao tunatoka out kwenda kula na wengine nasafiri nao kuwa nae mmoja pekee karibu ni sawa na kuwa hauna kabisa" Floyd Mayweather

Post a Comment

WRITE YOUR COMMENTS HERE

 
Top